Shimosaka Atsushi anayeishi mkoani Kyoto, alibainika kuumwa ugonjwa wa dimentia miaka mitatu iliyopita alipokuwa na umri wa miaka 46, akiwa katika kilele cha kazi zake. Anabainisha hisia na mawazo yake kuhusu kuishi na dimentia kwenye mitandao ya kijamii. Kupitia jumbe zake za mtandaoni tunapata kujua japo kwa uchache, kuhusu maisha yake na ugonjwa wa dimentia.
Shimosaka Atsushi alibainika kuumwa ugonjwa wa dimentia miaka mitatu iliyopita.
Atsushi kwa sasa anafanya kazi kama mtoa huduma katika kituo cha huduma kwa wazee nyakati za mchana.
Atsushi akiandika ujumbe maalum kwa mke wake Yoshiko kupitia mtandao wa kijamii.