Daktari mwenye asili ya Syria na Marekani Zahel Sahloul ni mwanzilishi wa Taasisi Isiyokuwa ya Kiserikali, NGO ya MedGlobal yenye makao yake mjini Chicago, ambayo imetuma wafanyakazi wa kujitolea na vifaa tiba katika maeneo yenye vita kote duniani ikiwemo Ukraine, na maeneo yaliyokumbwa na majanga ya asili. Tulimuuliza kipi kinachomsukuma kusaidia watu wanaokumbwa na mizozo. (Kipindi hiki kilitangazwa Februari 9, 2023.)