Ripoti: Semina ya Tafiti za Afya na Masuala ya Afrika
Hiki ni kipindi kinachohusisha mahojiano ya kusisimua na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya Japani. Wakati huu, tunakuletea ripoti kuhusu Semina ya Tafiti za Afya na Masuala ya Afrika iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa TKP uliopo Shimbashi jijini Tokyo nchini Japani.
Aidha, utasikiliza namna watangazaji wetu wanavyozamia gumzo za kuvutia zitakazokuacha ukivunjika mbavu. Hatimaye, kipindi kitafikia ukingoni baada ya sisi kutangamana nawe msikilizaji kwa kusoma ujumbe wako. Usikose kusikiliza!
(Kipindi hiki kilitangazwa Julai 30, 2023.)