Ripoti: Kongamano la kuadhimisha miaka 60 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Kenya na Japani
Hiki ni kipindi kinachohusisha mahojiano ya kusisimua na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya Japani. Wakati huu, tunakuletea ripoti kuhusu Kongamano la kuadhimisha miaka 60 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Kenya na Japani. Usikose kusikiliza!
Washiriki wa kongamano la kuadhimisha miaka 60 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Kenya na Japani.
Mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya NHK WORLD JAPAN, Mbozi Katala akiwa ameshika barakoa na maharagwe ya soya ikiwa ni ishara ya tukio la kitamaduni la setsubun nchini Japani ambapo watu hurusha maharagwe ya soya kama ishara ya kumfukuza shetani wakati wa kuingia msimu mwingine.