Vitu vya kuwekwa kwenye mfuko wa dharura vinaweza vikagawanywa katika makundi matatu. La kwanza linajumuisha vitu muhimu vya kuhakikisha uhai wako kama vile chakula na dawa. La pili ni bidhaa muhimu za matumizi kama vile tochi na shashi. Kundi la tatu linajumuisha vitu ambavyo ni vigumu kuvipata mara tu vipoteapo, kama vile nakala za vyeti vya ukaazi au orodha ya namba za simu za watu unaojuana nao.